Jun 19, 2017

Jitibu kwa kutumia MAJI tu!

Mambo ya kuzingatia kabla ya kuanza tiba kwa kutumia maji:
Ifuatayo ni kanuni ya jumla ya namna ya kuyatumia maji ya kunywa katika kujikinga na kujitibu na maradhi au magonjwa mbalimbali mwilini. Kwa sababu ili maji yawe ni dawa basi kuna kanuni ya kuyanywa maji hayo.

Kanuni ya kimakisio kwa mahitaji ya maji ni; kunywa nusu ya uzito wako katika aunsi (ounces) ugawe mara mfululizo utakaoufuata kwa siku nzima. Kiasi kidogo chini au juu ya hiki, kinakubalika. Aunsi 1 = miligramu 31.25.

Kanuni ya kimakisio kwa mahitaji ya chumvi ni, Robo tatu gramu za chumvi kwa kila nusu lita ya maji, nusu kijiko cha chakula kwa kila nusu galoni ya maji au kijiko kimoja cha chakula kwa kila galoni moja la maji.

Pengine umeshageuza kichwa na kujisemea, “Wewe ni kichaa…..hicho ni kiasi kingi sana cha maji”.

Ukweli ni kuwa, ni rahisi kunywa hivyo hasa tukitumia sentensi, glasi 8 za maji zikigawanywa mara nane kwa siku (glasi 1 = ml 250 au robo lita).
Mfano, kwa mtu mwenye uzito wa kilogramu 75:


  • Badili kilogramu kwenda aunsi kwa kuzidisha mara 2.2. Hivyo, 75×2.2 = aunsi 165.
  • Tafuta nusu ya aunsi kwa kugawa aunsi na 2. Hivyo, aunsi 165/2 = aunsi 82.5.
  • Gawanya mara mfululizo utakaoamua kuufuata kwa siku nzima, mfano mara 8 kwa siku. Kwa hiyo aunsi 82.5/8 = aunsi 10.3.
  • Badili aunsi kuwa miligramu za maji. Aunsi 1 = miligramu 31.25. Kwa hiyo aunsi 10.3×31.25 = miligramu 322.

Kwa hiyo itampasa mtu huyo mwenye uzito kilo 75, kunywa ml 322 za maji mara nane kwa siku.

Namna anavyopaswa kufuata hiyo ratiba mara 8 kwa siku:
1) Akiamka tu (mfano saa 12 kamili asubuhi), cha kwanza atakunywa maji ml 322. ataendelea na shughuli zake za asubuhi

2) Nusu saa kabla ya chakula cha asubuhi (yaani saa 12:30 asubuhi), atakunywa maji ml 322. atasubiri nusu saa ipite ndipo atapata chakula chake cha asubuhi (itakuwa saa 1 kamili asubuhi).

3) Kisha kula chakula cha asubuhi, atahesabu masaa 2 na nusu ndipo atakunywa tena maji ml 322 (itakuwa saa 3 na nusu asubuhi).

4) Atahesabu masaa 2 tena ndipo atakunywa tena ml 322 nusu saa kabla ya chakula cha mchana (itakuwa saa 6 mchana) kwa hiyo nusu saa baadaye atakula chakula cha mchana (yaani saa 6 na nusu mchana).

5) Atahesabu yapite masaa 2 na nusu baada ya chakula cha mchana ndipo atakunywa tena maji ml 322 (itakuwa saa 9 kamili alasiri).

6) Atahesabu masaa 2 na nusu yapite ndipo atakunywa maji ml 322 nusu saa kabla ya chakula cha jioni (itakuwa saa 11 na nusu jioni). Nusu saa baadaye atakula chakula cha jioni (itakuwa saa 12 kamili jioni).

7) Kisha kula chakula cha jioni, atahesabu masaa 2 na nusu tena ndipo atakunywa tena maji ml 322 (itakuwa saa 2 na nusu usiku).

Muda wowote atakapokwenda kulala kuanzia saa 4 usiku atakunywa tena maji ml 322 kumalizia mara 8 zake kwa siku.

Huyo alikuwa na kilo 75, sasa na wewe andika uzito wako na utumie fomula hiyo hapo juu ujuwe ni kiasi gani cha maji unahitaji kwa siku na kisha ufuate mara hizo 8 kama zilivyopendekezwa hapo juu. Kwa staili hii ndipo maji huwa ni zaidi ya dawa.

Kila mmoja wetu sasa anaweza kutumia uzito wake kwa kutumia fomula hii na kujua ni kiasi gani cha maji anahitaji kwa siku.

Kumbuka, Kunywa maji nusu ya uzito wako katika aunsi ni kiasi cha chini kabisa, lakini mahala pazuri pa kuanzia, ikiwa ni mtu unayejishughurisha zaidi na mazoezi au unaishi katika mazingira ya joto zaidi, utahitaji zaidi ya hapo.

Sasa, hutakubali kuwa kunywa maji kwa protokolo hii ni kazi rahisi?.
Ikiwa haunywi kiasi hiki cha maji kwa sasa, unapaswa kuanza kuongeza kiasi cha ziada kwa taratibu sana. Hii itaupa nafasi mwili kujirekebisha kuendana na kiasi ulichoanza kukiongeza, na ikiwa hautaupa mwili muda wa kujirekebisha, basi maji yatakuwa kama dawa ya kukojosha (diuretic), yakisukuma madini na vitamini za mhimu nje ya mwili, pengine na kukusababishia madhara zaidi kuliko faida.

Watu wazee na watoto wadogo wanatakiwa kuanza kuongeza maji kufikia mahitaji yao kwa taratibu zaidi.

Kwa kutumia mfano wa uzito hapo juu, itakupasa kuanza na glasi 3 siku ya kwanza huku ukiongeza glasi moja zaidi kila siku inayofuata mpaka ufikie glasi zote 8.

Kumbuka kuwa, kunywa maji nusu ya uzito wako katika aunsi na kula chumvi robo tatu gramu kwa kila nusu lita ya maji, ni kanuni ya kimakisio tu. Baadhi ya wengine watahitaji maji zaidi wakati wengine watahitaji chumvi zaidi. Baada ya muda, mahitaji ya mwili kwa maji na chumvi yanaweza kuongezeka kidogo zaidi sababu ya mazingira ya joto, mazingira ya baridi au mazoezi ya viungo.

Kila mmoja lazima apate kujua kiasi cha mahitaji ya mwili wake kwa maji kuanzia sasa.

Kamwe usinywe zaidi ya aunsi 33.8 (lita moja) za maji kwa wakati mmoja ukiwa umekaa au umesimama.

Watoto wadogo kuanzia miaka 2 mpaka 12, hasa wale wepesi kujishughulisha na mazoezi wanahitaji asilimia 75 mpaka 100 za aunsi za maji katika uzito wao kwa sababu miili yao inakua muda wote na kila seli katika miili yao inayokua inayahitaji maji haya ya ziada (mytosis).

Tiba hii ya maji haitumiki kwa watoto chini ya miaka 2.

Chumvi ya kawaida ya mezani iliyoongezwa madini ya iodini, itakusaidia kidogo, chumvi ya mawe ya baharini ambayo haijasafishwa (unrefined sea salt) ndiyo nzuri zaidi sababu ya madini mengine mengi ya ziada zaidi ya 80 yaliyomo ndani yake. Chumvi ya baharini pia huwa na radha nzuri, nyeupe na umajimaji kidogo.

Namna bora za kula chumvi:
Njia ya kwanza ni kuiweka chumvi katika sehemu ya mbele ya ulimi, hakikisha unaihisi radha yake, na kisha kunywa maji juu yake yakiisafisha kuelekea chini.

Unaweza pia kuongeza chumvi ya ziada kwenye chakula chako.Tatizo la njia hii ni kuwa, chakula kinahisika kuwa na chumvi zaidi ya radha zingine.

Ukiona viwiko, vidole, miguu, mikono au kope za macho zinavimba (kuvimba kusikotokana na ajali au jeraha), au unaharisha zaidi, usitumie chumvi kwa siku 2 mpaka 3, kunywa maji halisi pekee na kisha siku ya tatu, endelea kuchukuwa chumvi tena, lakini ichukuliwe taratibu. Kamwe usitumie chumvi zaidi ya robo tatu gramu kwa kila nusu lita ya maji.

Kumbuka chumvi ikizidi hupelekea kuharisha.
Dr.Batmanghelidj anasema, kunywa maji matupu kunaweza pelekea mwili kupoteza baadhi ya madini na vitamini zake mhimu nje ya mwili na hivyo kutozipa seli muda wa kutosha kuyatumia maji. Inashauriwa kutumia vidonge vyenye vitamini nyingi kwa pamoja (multivitamins) katika kila mlo wako ili kurudishia kile kitakachokuwa kimepotea (hasa ikiwa haufanyi mazoezi na kula kiasi kingi cha mboga za majani).

Uvimbe utakapokuwa umepotea au umeacha kuharisha, unaweza kuendelea na mpango wako wa kunywa maji nusu ya uzito wako katika aunsi ingawa mara hii utayachukua kwa kiasi kidogo.

Kwa siku nzima, anza kuongeza kiasi cha unywaji wako wa maji mpaka ufikie tena nusu ya uzito wako katika aunsi, anza pia kuchukua chumvi pamoja na maji. Unatakiwa kuhakikisha kuwa unapata gramu 150 za madini ya iodine kwenye “multivitamins” zako kila siku mpaka gramu 450 kwa siku.

Kisha kunywa maji, maji yanapaswa kubaki ndani ya mwili masaa 2 mpaka 2 na nusu ili kuupa mwili muda wa kutosha kuyatumia maji hayo vizuri.

Ikiwa inakulazimu kukojoa (peeing) chini ya muda wa masaa 2 tangu unywe maji, utalazimika kuacha kunywa maji matupu, jaribu kunywa juisi (uliyotengeneza mwenyewe) ya chungwa, ya limau au ya zabibu au juisi nyingine yeyote isipokuwa kwa watu wanaosumbuliwa na pumu (asthma) ambao hawatakiwi kunywa juisi ya chungwa.

Wakati huo huo mhimu kukumbuka kuongeza robo 

Jun 16, 2017

Mwanamke anayeifaa NDOA!

UHALISI WA MAISHA:
Maisha halisi ya mwanamke anayetarajia kuwa mke/ mke tayari hii ni kumaanisha kuwa wanawake mashujaa tunapaswa kuishi maisha ambayo yanatutambulisha kama mfano wa kuigwa ili tunapozungumza na kufundisha mabadiliko tuwe tunazungumza uhalisia wa maisha yetu ambao unajengwa na haya yafuatayo;

UVUMILIVU:
Kuwa mvumilivu katika maisha yake ya kila siku hasa ukizingatia kuwa tunakutana na mambo mbali mbali yasiyotuvutia katika mahusiano yetu, mengine ni magumu na yanayokwenda kinyume kabisa na matakwa yetu au mazoea yetu ya binafsi. Ifahamike kwamba wewe kama mwanamke shujaa inapotokea umekutana na mambo kama haya hupaswi kuonyesha hasira zako wazi wazi kama vile; chuki, kulaumu, ugomvi, vurugu, malalamiko, manung’uniko, machafuko, kulipa kisasi au aina yoyote ya uharibifu kutokea kwako au ndani mwako. Hivyo mwanamke shujaa huwa ni heri kila anapokuwa kwani hutunza amani ya eneo alipo.

UPENDO WA DHATI:
Maisha ya upendo wa halisi na sio wa kinafki kwa jamii inayomzunguka. Tabia ya upendo wa halisi ina thamani kubwa sana kuliko mali nyingi, pesa, elimu ya juu n.k. wewe unaweza kabisa kuwa na elimu ya juu sana na pesa nyingi sana lakini pasipo upendo wa halisi ni sawa na kusema kopo zuri kwa nje na ndani hamna kitu. Nguzo kuu ya maisha ya mwanamke shujaa ni Upendo wa dhati na uhalisia.

UTII KWA KWA JAMII:
Maisha halisi ya utii katika jamii inayokuzunguka  ili kuweza kuyafanyia kazi yale yote uliyojifunza na pia kuyatenda kwa ufasaha pasipo kupita kona yoyote. Utii  kwa jamii ni ufunguo mmoja wapo utakaokusaidia kufanikisha mambo yako na malengo yako kama mwanamke shujaa.

UAMINIFU KATIKA JAMII:
Kuishi maisha ya uaminifu wa kweli na uhalisia katika jamii inayomzunguka. Uaminifu wa kweli huonekana nyakati zote na siyo tu wakati mtu anapokuwa mbele za watu wanaomjua bali hata wale wasiomjua na hata anapokuwa mahali peke yake aweze kutunza uaminifu wake kwa faida ya jamii nzima. Mwanamke shujaa hujitahidi sana kutunza uaminifu wake katika sekta zote.

UNYENYEKEVU WA KWELI:
Kuishi maisha halisi kabisa ya unyenyekevu kwa jamii inayomzunguka, unyenyekevu ni kinyume kabisa na kiburi, majivuno, kujigamba, kujikweza, kujiinua, kujiona,na hata kjitanguliza mbele kwa kila jambo. Mwanamke shujaa huwa ni mnyenyekevu wakati wote na hana makuu daima.

UWAJIBIKAJI WA DHATI:
Maisha halisi ya uwajibikaji akiangalia majukumu yake yote yanayomkabili na kuhakikisha anafanya kwa moyo bila kuwa na tabia ya kusaidiwa majukumu yake. Mwanamke shujaa ni mfano wa kuigwa kutokana na uwajibikaji wake.

USHIRIKIANO WA DHATI:
Ushirikiano katika jamii inayomzunguka. Sisi wanawake mashujaa yatupasa kujua dhahiri kuwa kazi ya kubadili tabia na kufanya wengine wabadilike kwa lengo la kupata familia bora ni lazima kuwa na ushirikiano wa kweli ambao utajenga tabia ya kuaminiana na kunai mamoja katika harakati hizi za kuandaa/ kujenga familia bora.

UTARATIBU WA KAZI/MPANGILIO:
Katika utaratibu wa maisha yake, pamoja na mpangilio mzuri wa mambo yanayomzunguka hii itakusaidia kuwa na muda mzuri wa kufanya shughuli zako na pia kutekeleza majukumu yako ya kila siku kama mwanamke shujaa. Hakuna njia yoyote ya kukuwezesha kukua na kuendelea katika maisha yako bila kuwa na utaratibu na mpangilio wa mambo yako.

KUFANYA TATHIMINI:
Kuweza kufanya tathimini ya yale yote anayoyafanya katika maisha yake ya kila siku, pengine ni mfanyabiashara, mfanyakazi, mkulima n.k kama mwanamke shujaa yakupasa kutathimini shughuli zako kama zina leta faida/hasara kwa familia na jamii yako inayokuzunguka. Ukiona faida ni kubwa unaendelea na hiyo shughuli lakini kama hasara ni kubwa unajiweka katika nafasi ya kubadilisha aina ya shughuli mara moja bila kupoteza wakati.

Jun 14, 2017

Nimeipata InBox kwangu, Lol!

Mapenzi kama siasa, usipo ongea uongo hupati kura wala hapendwi mtu bila kitu na anaekuita baby ndio atakae kuita babu siku ukifulia, jipange mtu wangu maisha magumu na umri haurudi nyuma, hakuna tuzo za ngono zaidi ya UKIMWI. Acha tamaa na mapenzi yatakupoteza na usione unapendwa sana na wanawake au wanaume ukajiona ndo mwanaume/mwanamke bora kuliko wengine, huenda una nyota ya UKIMWI, Hii sms watumie wapiga misele kwa mademu/Wanaume wote, kwangu ilitumwa kimakosa. Hahahaa.. Ab.

Feb 9, 2014

Enjoy NU Audio: Khalifa Juma (CT) - "NEXT LEVEL"

Baada ya kutinga jijini Dar es salaam na EBSS 2013, Ingawa alishindwa kuingia Top 20, ila ilikuwa poa sana. Na hii ni ngoma yake mpya kati ya alizowahi kuzitoa kimtaa. Sipport mziki wake kwa kudownload ngoma hiyo hapa...

Jan 30, 2014

Pictures: Hii ni zaidi ya Catoon, Check Out

 Click hapa chini kutizama picha zaidi...

Daah! Mwandishi mwingine wa BBC afariki dunia

Mwandishi wa BBC Ann Waithera afariki
Mwandishi wa BBC nchini Kenya Ann Waithera ameaga dunia akiwa na umri wa miaka 39 baada ya kuugua Saratani kwa muda mrefu..

Gosby kufanya "SCARFACE VALENTINE'S DAY MASSACRE II" na Hiki ndicho alichokisema FB

 Gosby kufanya "SCARFACE VALENTINE'S DAY MASSACRE II" Hiki ndicho alichokisema katika ukurasa wake wa FaceBook.......
Nafanya mixtape SCARFACE VALENTINE'S DAY MASSACRE 2, unadhani rapper gani ahusike na yeye kwenye hii mixtape janangu ashushe bars..

LAMAR: Soon kuanzisha kipindi cha uhalisia wa kazi zake akiwa STUDIO na mengineee

Kwa story zaidi kuhusiana na hili tembelea Bongo5 kwa kubofya HAPA!

Steal New: Msami - Soundtrack (Official Video)

Jan 27, 2014

T was #FamilyDay ya HighlandsFM @ ManyanyaInn, Ilikuwa poa sana, checkna hizi Pics Kadhaa

 Check na pics zangu kadhaa kucheck ilivyokuwa...
Angalizo: Hii ni blog yangu binafsi, hivyo naweza kufanya lolote  nitakalo..

Jan 26, 2014

Leo katika Historia, Miaka 114 iliyopita, kutoka Iran

Siku kama ya leo miaka 114 iliyopita mfamasia wa Kijerumani Felix Hoffmann alitengeneza dawa ya kwanza ya kutuliza maumivu. Dawa hiyo hii leo inajulikana kwa jina la Aspirin. Waingereza pia waliamua kutengeneza dawa hiyo katika kipindi cha Vita vya Kwanza vya Dunia baada ya uingizaji dawa hiyo nchini Uingereza kusimamishwa. Mbali na kutuliza maumivu, Aspirin ina sifa nyingine kadhaa ambazo ni pamoja na kuzuia damu isigande na kuzuia mshtuko wa moyo.

Jan 12, 2014

Wanyaka majambazi sugu Katavi, yakiwa na bunduki za KIVITA. KIVITAAAH!!!!



JESHI la Polisi Mkoa wa Katavi linawashikilia watu 3 kwa tuhuma za kukutwa na bunduki ya kivita aina ya G3, ikiwa na risasi zake tisa wakati wakisafirisha silaha hiyo kutoka Mpanda kuelekea Tunduma, Mbeya.
Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Katavi, amewataja watuhumiwa  waliokamatwa kuwa ni  Simon Kasobhile, maarufu kwa jina la Kamwela mkazi wa Ileje, Mbeya. Wengine ni Bilau Rashid, maarufu kwa jina la Maftah, mkazi wa Rukwa  na Martine John mkazi wa Tunduru, waliokamatwa Januari 10, majira ya usiku katika Kitongoji cha Matandalani, Kata ya Sitalike, wilayani Mlele.
Kwa mujibu wa kamanda Kidavashari, watu hao walikamatwa  wakiwa kwenye gari aina ya Toyota  Cruiser Prado,  lenye namba za usajili T 564 ABW lililokuwa likiendeshwa na George Kiluli, mkazi wa Mpanda. Amesema  dereva wa gari hilo alikuwa anampeleka mdogo wake, Gabriel Samwel, Shule ya Sekondari Laela, Sumbawanga na alipofika eneo la City mjini Mpanda alisimamisha gari na kupakia abiria wakiwamo watuhumiwa hao.

KIFO cha Kagame, Wa2 wa Rwanda wafanya sherehe

Kwa masaa kadhaa Ijumaa nyakati za asubuhi, kulikuwa na fununu kuwa Rais wa Rwanda, Paul Kagame ameaga dunia na taarifa hizo zilienea hadi mji wa Goma Mashariki mwa Congo. Wengi walisherehekea baada ya kupata habari hizo.

MSIBA: TAJI Liundi afiwa na baba yake mzazi, R.I.P our papaa Jaji George Bakari Liundi



ATANGAZA TAARIFA LEO
TAARIFA YA MSIBA: Nasikitika kutangaza kifo cha Baba Mzazi Jaji George Bakari Liundi kilichotokea ghafla leo Jumapili saa 7 mchana. 
Msiba upo KEKO JUU KJ 60(Nyuma ya Mgulani Shule ya Msingi). 
Taratibu za mazishi zinaendelea. 
Mawasiliano: 0787 888 799.

Jan 10, 2014

Yaya Toure atwaa tuzo ya mwanasoka bora Afrika '13

Mchezaji wa kati wa timu ya soka ya Manchester City ya Uingereza, Yaya Toure, amenyakua tuzo ya mchezaji bora wa mwaka wa Shirikisho la Soka la Afrika, CAF.

Mchezaji huyo wa kimataifa wa Ivory Coast amenyakua tuzo hiyo na kuwapiku washindani wake wawili Didier Drogba anayesakata kabumbu katika timu ya soka ya Galatasaray ya Uturuki na kiungo wa Chelsea na timu ya taifa ya Nigeria John Obi Mikel.

Hii ni mara ya tatu mfululizo kwa Yaya Toure kushinda tuzo ya mchezaji bora wa CAF, baada ya mwaka 2011 na 2012 kujinyakulia pia tuzo hiyo. Wakati huo huo kocha wa timu ya soka ya taifa ya Nigeria Stephen Keshi amenyakua tuzo ya kocha bora wa mwaka barani Afrika katika soka.

Katika sherehe za kuwatangaza waliong'ara katika soka barani Afrika mwaka 2013 huko Lagos Nigeria, Keshi alishinda tuzo ya kocha bora.

Jan 7, 2014

Historia: Siku kama ya leo miaka 690 Iliyopita

Siku kama ya leo miaka 690 alifariki dunia mtalii mashuhuri wa Kiitalia Marco Polo. Alizaliwa katika mji wa Venice nchini Italia na alianza safari iliyokuwa na mikasa mingi akiwa na umri wa miaka 18 akiwa pamoja na baba yake. Safari ya kitalii ya Polo katika nchi za Mashariki iliendelea kwa kipindi cha miaka 20.
Alirejea nchini Italia mwaka 1291 na kuandika aliyoyaona katika kitabu alichokipa jina la "Maajabu". Kitabu hicho kilipata umashuhuri mkubwa duniani na alizungumzia kwa mapana na marefu kuhusu aliyoyaona katika nchi za China, Turkemanistan, Mongolia na sehemu za kusini mashariki mwa Asia.
Siku kama ya leo miaka 372 iliyopita alifariki dunia msomi mashuhuri, mnajimu na mtaalamu wa fizikia wa Italia Galileo Galilei akiwa na umri wa miaka 78.
Alizaliwa katika mji wa Pisa na alisoma fasihi hadi alipokuwa na umri wa miaka 19 na baadaye akajishughulisha na fizikia na hisabati. Galileo alitumia lenzi iliyovumbuliwa na msomi na mnajimu mashuhuri wa Kiislamu, Ibn Haitham kutengeneza darubini ya elimu ya nujumu kwa ajili ya kutazamia nyota na sayari

Jan 5, 2014

UPDATES: MV Kilimanjaro, 5 wafa, wengine HOFU!!

WATU kadhaa wanahofiwa kupoteza maisha ikiwa 5 wathibitishwa kufa baada ya boti ya MV Kilimanjaro 2 inayomilikwa na shirika la Azam Marine kukumbwa na dhoruba katikati ya bahari, wakati ilipokuwa safarini kutoka kisiwani Pemba kuelekea kisiwani Unguja.
Baadhi ya habari nchini Tanzania zimelinukuu jeshi la polisi likidai kuwa, baadhi ya abiria waliokuwemo kwenye boti hiyo walichukua majaketi ya kujiokolea na kuyatupa nje ya boti hiyo.
Hata hivyo watu mbalimbali waliokuwemo kwenye boti hiyo walipohojiwa na vyombo vya habari wamesema kuwa majaketi yaliyokuwemo yalikuwa hayatoshi na watu waliyapata kwa kugombania.
Hadi hivi sasa idadi hasa ya watu waliopoteza maisha yao haijajulikana. Taarifa zinaongeza kuwa, boti hiyo ilikuwa na abiria 69 watu wazima, abiria watoto 60 na mabaharia wanane.
Iliondoka saa mbili asubuhi kisiwani Pemba kuelekea kisiwani Unguja, na ilipofika katika eneo la Nungwi bahari ilichafuka na boti ikaanza kuyumba.

Jan 2, 2014

LEO katika Historia, Miaka 1435 iliyopita...


Siku kama ya leo miaka 1435 iliyopita, Mtume Muhammad SAW alianza Hijra yake ya kuhama Makka na kuelekea Madina, ikiwa imepita miaka 13 tokea alipobaathiwa na kupewa Utume. Mtume wa Allah alihajiri Makka kutokana na kushadidi vitimbi vya washirikina wa mji huo ambao walikusudia kumdhuru na kumuua wakati wa usiku akiwa amelala nyumbani kwake. Imam Ali AS alijitolea mhanga, kwa kuamua kulala kwenye kitanda cha Mtume, ili maadui wasitambue kwamba Mtume wa Allah tayari ameshaondoka mjini Makka. Inafaa kuashiria hapa kuwa, tukio la kuhajiri Mtume SAW lilikuwa ni mwanzo wa kalenda ya Kiislamu, kwani barua zote zilizokuwa zikipelekwa kwa wakuu wa makabila na shakhsia maarufu zilikuwa zikiandikwa kwa kufuata kalenda hiyo.Siku kama ya leo miaka 1370 inayosadifiana na tarehe Mosi Rabiul Awwal mwaka 65 Hijria, ilianza harakati ya Tawwabin kwa lengo la kulipiza kisasi cha kuuawa shahidi Imam Hussein AS pamoja na wafuasi wake watiifu. Awali, watu wa Kufa walimuomba Imam Hussein AS aelekee mjini humo kwa lengo la kuongoza harakati dhidi ya utawala wa kidhalimu wa Yazid bin Muawiya. Tawwabin ni kundi la watu wa Kufa ambalo lilijuta kwa kushindwa kutekeleza ahadi zake na kumuacha Imam Hussein na wafuasi wake wachache peke yao wapambane na majeshi ya Yazid. Kwa minajili hiyo watu hao walitubia makosa yao na kuamua kuanzisha harakati ya kulipiza kisasi wakiongozwa na Suleiman bin Sorad dhidi ya jeshi la Yazid.

Siku kama ya leo miaka 21 iliyopita, inayosadifiana na tarehe 3 Januri 1993, yalitiwa saini  makubaliano ya kupunguza silaha za atomiki kati ya Boris Yeltsin, Rais wa zamani wa Russia na George Bush 'baba', Rais wa zamani wa Marekani. Kwa mujibu wa makubaliano hayo, nchi hizo mbili zilipaswa kupunguza theluthi mbili za silaha zao za atomiki. Hata hivyo, mnamo mwezi Aprili mwaka 2010 Russsia na Marekani zilitiliana saini makubaliano mapya ya START ambayo yalikuwa na lengo la kupunguza vichwa vya makombora 1,550 ya nyuklia.
Na siku kama ya leo miaka 25 iliyopita, inayosadifiana na tarehe 13 Dei 1367 Hijria Shamsia, Imam Khomeini (MA) Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu alimtumia ujumbe Mikhail Gorbachev, Rais wa mwisho wa Urusi ya zamani akimtaka  asilimu na kuachana na fikra za Kimaksi. Ujumbe huo wa Imam Khomeini MA ulipelekwa na Ayatullah Jawad Amoli, mmoja wa maulama wakubwa hapa nchini.

Dec 22, 2013

Bishop Joe: KUWENI NA HOFU YA MUNGU katika Kuumaliza mwaka huu na kuanza vema mwaka 2014


WANANCHI wametakiwa kuwa na hofu ya Mungu katika kipindi hiki cha kuumaliza na kuuanza mwaka mpya wa 2014 kwa kudumisha amani na utulivu ili kuvuka kwa usalama.

Wito huo umetolewa na Askofu wa makanisa ya Bread of Life, Joe Imakando, wakati akiongea na Highlands FM katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Songwe mkoani Mbeya.

Askofu Imakando ameeleza kuwa watu wanatakiwa kuwa karibu na huduma za kidini ili kuimarisha amani na usalama katika kipindi hiki na kusema kuwa watu wanatakiwa kulinda amani yao wao wenyewe.

Pia amesifia uongozi wa kisiasa na serikali ya nchi ya Tanzania kwa kusema kuwa ni bora kwani wanatatua matatizo yao bila ya kusababisha uvunjifu wa amani.

Dec 14, 2013

New TOYOTA ALTEZZA hii hapa, 7.5 Millon


TOYOTA ALTEZZA
car on the road: 7 500 000 tsh (not negotiable)
Mileage 72,842
Model Code GF-SXE10
Registration
Year/month 1999/6
Manufacture
Year/month 1999/6 
Version/Class RS200
Chassis # SXE10-0026649
Engine Size 1,990cc
Engine Code 3S
Drive -
Ext. Color Silver
Steering Right
Transmiss. Automatic
Fuel Gasoline/Petrol
Seats 5
Doors 4

Sometimes Think about T @#$%$$#$%%*) #!@#$%


DIAMOND PLATUNUMZ: Asanteni kwa kuwa nami ktk #CokeStudioAfrica


KATIKA ukurasa wake wa FaceBook Diamond Platnumz ameandika hivii.....
Asanteni sana kwa kuungana nami kwenye Coke Studio Africa 
Watch out for the NEW videos ambazo watazitoa hivi karibuni. Asanteni tena sana!