Jan 12, 2014

Wanyaka majambazi sugu Katavi, yakiwa na bunduki za KIVITA. KIVITAAAH!!!!



JESHI la Polisi Mkoa wa Katavi linawashikilia watu 3 kwa tuhuma za kukutwa na bunduki ya kivita aina ya G3, ikiwa na risasi zake tisa wakati wakisafirisha silaha hiyo kutoka Mpanda kuelekea Tunduma, Mbeya.
Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Katavi, amewataja watuhumiwa  waliokamatwa kuwa ni  Simon Kasobhile, maarufu kwa jina la Kamwela mkazi wa Ileje, Mbeya. Wengine ni Bilau Rashid, maarufu kwa jina la Maftah, mkazi wa Rukwa  na Martine John mkazi wa Tunduru, waliokamatwa Januari 10, majira ya usiku katika Kitongoji cha Matandalani, Kata ya Sitalike, wilayani Mlele.
Kwa mujibu wa kamanda Kidavashari, watu hao walikamatwa  wakiwa kwenye gari aina ya Toyota  Cruiser Prado,  lenye namba za usajili T 564 ABW lililokuwa likiendeshwa na George Kiluli, mkazi wa Mpanda. Amesema  dereva wa gari hilo alikuwa anampeleka mdogo wake, Gabriel Samwel, Shule ya Sekondari Laela, Sumbawanga na alipofika eneo la City mjini Mpanda alisimamisha gari na kupakia abiria wakiwamo watuhumiwa hao.