Nov 30, 2010

Msiambukize Ukimwi makusudi.

KATIKA maadhimisho ya siku ya Ukimwi, Wakazi wa jijini na mkoa wa Mbeya wamelalamikia vitendo vya waathirika wa Ukimwi kusambaza ugonjwa huo kwa makusudi kwa dhana iliyojengeka kuwa ‘’Tufe wengi’’.
 Wakiongea na mwandishi wetu kwa nyakati tofauti kwenye viwanja vya Luanda Nzovwe kulikofanyika maaadhimisho hayo kimkoa walilalamikia suala hilo kwa huzuni huku wakiwasihi wenye tabia hizo kuacha mara moja.
 ‘’Kweli unaweza kuishi muda mrefu na maambukizo ya Ukimwi lakini sio iwe sababu kusambaza hata kama unaogopa watu wajue kuwa umeathirika basi tutumie zana (kondom)’’ alisema mkazi mmoja.
 Bi Helena Julius, yeye amejiunga na shirika la (SHIDEFA) linalojihusisha na kutoa elimu kwa waathirika wa Ukimwi ambapo yeye anaishi na maambukizo ya Ukimwi tangu Agosti mwaka 2005.
 Nao wamelizungumzia suala hilo na kuwa hiyo imekuwa ni moja kati ya changamoto kwao na kwamba wanajitahidi kadri ya uwezo wao ingawa bado kunakuwa na watu wasiokuwa waelewa.
 ‘’Nawasihi watu wawe waelea juu ya janga hili na waone kama kulitokomeza inawezekana’’ alisema Helen Julius.

Korea Kusini yafuta mazoezi ya kijeshi

Serikali ya Korea Kusini imetangaza kufutiliwa mbali mazoezi ya kijeshi ambayo yangehusisha matumizi wa silaha, katika kisiwa kilichoshambuliwa na wanajeshi wa Korea Kaskazini wiki iliyopita.
Korea Kusini yafuta mazoezi ya kijeshi
Korea Kusini yafuta mazoezi ya kijeshi

Jeshi la nchi hiyo limesema mazoezi hayo ni sehemu ya mazoezi ya pamoja yanayoendelea kati ya nchi hiyo na Marekani.
Hata hivyo hakuna sababu yoyote iliyotolewa kuhusu sababu zilizosababisha harakati hizo za mazoezi ya kijeshi zifutiliwe mbali.
Utawala wa Korea Kaskazini umesema mazoezi hayo yanayohusisha ufyatuaji risasi yalichochea uamuzi wake wa kushambulia kisiwa cha Yeonpyeong island siku ya jumanne wiki iliyopita.
Rais wa Korea Kusini, Lee Myungt Bak amesema atakabiliana vikali na serikali ya Korea Kaskazini endapo itajaribu kufanya mashambulio kama hayo.

Nov 24, 2010

ZAIDI YA WATU 378 WAPOTEZA MAISHA CAMBODIA

WATU wasiopungua 378 wamepoteza maisha  na wengine 755 kujeruhiwa baada ya kukanyagana katika daraja la mto Bassac baada ya hofu kuzuka wakati wa Sherehe za Maji nchini humo. Waziri Mkuu wa nchi hiyo Hun Sen alisema  tukio kama hilo halijawahi kutokea tangu miaka ya 1970 enzi za utawala wa  Khmer Rouge ya mapema jana jumatata kuwa leo yaani Jumanne itakuwa ni siku ya kutambua miili ya marehemu na kuongeza kuwa Juhudi za kuitafuta miili miingine zinaendelea katika mto huo.


Waziri huyo alitangaza kuwa siku ya Alhamis itakuwa siku ya Maombolezo nchini humo na Mamlaka husika zimetakiwa kushusha bendera nusu mlingoti ifikapo siku hiyo na kusema kuwa  Serikali ya nchi hiyo itazilipa familia zilizofikwa na msiba kwa mtu liyekufa itatoa dola 1250 sawa na shilingi milioni 2 za kitanzania  gharama za mazishi na kwa kila aliyejeruhiwa  kiasi cha dola 250 sawa na kiasi cha shilingi laki tatu.
Pole kutoka kwa Abbin Mbungula.