Aug 31, 2012

KILICHOSEMWA NA CHAMA CHA WAALIMU TANZANIA

Chama cha walimu (CWT) kimesema pamoja na bunge la Jamuhuri ya muungano wa Tanzania na Mahakama kuagiza chama hicho na serikali kurudi kwenye meza ya mazungumzo kwa lengo la kuyapatia ufumbuzi madai ya walimu, bado serikali haijaonyesha utayari wowote wa kufanya hivyo.

Rais wa CWT Gratian Mukoba amesema chama kimechukua hatua mbalimbali ikiwemo kumwandikia barua katibu mkuu kiongozi zaidi ya mara moja kuonyesha utayari wa CWT kukutana na Serikali kwa majadiliano lakini hadi sasa hakuna taarifa yoyote kutoka serikalini.

Amesema kitendo cha serikali kukaa kimya kwa muda wa siku 27 bila kuonyesha kujali kutekelezwa kwa amri ya Mahakama, kinatafsiriwa na CWT kama ni kukosekana kwa nia njema ya serikali kusikiliza madai ya walimu.

Kwenye line nyingine, CWT kimeitaka serikali kuwaachia huru baadhi ya viongozi wa CWT na walimu wote waliofunguliwa mashtaka ikiwa ni pamoja na kuwarejeshea madaraka walimu 15 waliovuliwa vyeo vyao kutokana na mgomo wa walimu.

KWA NINI BEB POL HATAKI COLLABO?

Msanii anayeondoka na style za RnB hapa bongo, huyu si mwingine namzungumzia  Ben pol.

Msanii huyu amesitisha kufanya collabo na wasanii mpaka amalize project ya nyimbo yake inayofahamika kwa jina la Pete.

Ben ameeleza kwamba utakuta anatumia muda mwingi sana katika kufanya collabo na wasanii wa hapa nchini na hicho ndicho kinachomfanya asimalize project zake.

Kwa hiyo amesitisha kwanza mpaka amalize project yake ya pete ndipo atachukua uamuzi wa kufanya collabo na wasanii.

 Hayo ndiyo maneno ya Ben Pol akifunguka kuhusiana na sababu za kutokufanya collabo.. KILA LA KHERI BEN POL..

MSANII CHRIS AJIUA

Mwanzilishi na mmiliki wa Violator Entertainment anayefahamika kwa jina la Chris Lighty ambaye pia alikuwa mwanamuziki wa HipHop amefariki dunia siku ya jana huko Marekani baada ya kujipiga risasi.

Chriss amejiua kutokana na tafrani iliyokuwa ikimsumbua baina yake yeye na mkewe chanzo kikiwa ni upotevu wa fedha na madeni yanayoikabili familia hiyo.

Chris ambaye alikuwa akidaiwa Dola Milioni Tano ($5 m.) na IRS alilazimika kuuza baadhi ya vitu vyake ikiwa pamoja na hotel ili kuweza kulipa deni hilo hali iliyomfanya kuonekana kama amechanganyikiwa na muda mwingi walikuwa hawaelewani na mkewe Veronica.

Chris hatasahaulika kwa kuviinua vipaji ambavyo kwa sasa ndio nguli wa muziki duniani kama vile; 50 Cent, Maria Carey, Busta Rhymes, Diddy, Jarule na wengine KIBAOOO. RIP MAN..

Aug 30, 2012

HAYA NDIO MAJINA HALISI YA WASANII WETU

Crazy GK ------------------Gwamaka Kaihula 
Ngwea---------------------Albert Mangwea 
Maunda -----------Maunda Zahir Ally Zoro
Banana------------Banana Zahir Ally Zoro
TID --------------------Khalid Mohamed
Prof Jay----------------------Joseph Haule
Belle 9----------------------------Aberenego
Ommy Dimpoz--------- ---Omary Faraji Nyembo
Linex -------------------------Linex Sunday Mjeda
Chege-----------------------------Said Juma Hassan
Fid Q-----------------------------Fareed Kubanda
Diamond-------------------------Abdul Naseeb
Dogo janja-----Abdul-aziz Abubakar Chende
Jaffarai------------------Jaffar Msham Ally
Shilole---------------Zuwena MUhhamed
Nikki wa pili ------------Nickson Simmon
Joe Makini --------------------John Simmon
G nako --------------------------George Sixtus
PNC------------------Pancras Chaz Ndaki
AY-------------------Ambwene Yesaya
FA---------------Hamis Mwinjuma
Juma Nature ---Juma Kassim Kiroboto
Q chief ----------Abubakar Shaaban Katwila
Ray c ------------------------Rehema Chalamila
Jay dee-----------------------------Judith Wambura
Jay moe-----------------------------Juma mchopanga