Jan 10, 2014

Yaya Toure atwaa tuzo ya mwanasoka bora Afrika '13

Mchezaji wa kati wa timu ya soka ya Manchester City ya Uingereza, Yaya Toure, amenyakua tuzo ya mchezaji bora wa mwaka wa Shirikisho la Soka la Afrika, CAF.

Mchezaji huyo wa kimataifa wa Ivory Coast amenyakua tuzo hiyo na kuwapiku washindani wake wawili Didier Drogba anayesakata kabumbu katika timu ya soka ya Galatasaray ya Uturuki na kiungo wa Chelsea na timu ya taifa ya Nigeria John Obi Mikel.

Hii ni mara ya tatu mfululizo kwa Yaya Toure kushinda tuzo ya mchezaji bora wa CAF, baada ya mwaka 2011 na 2012 kujinyakulia pia tuzo hiyo. Wakati huo huo kocha wa timu ya soka ya taifa ya Nigeria Stephen Keshi amenyakua tuzo ya kocha bora wa mwaka barani Afrika katika soka.

Katika sherehe za kuwatangaza waliong'ara katika soka barani Afrika mwaka 2013 huko Lagos Nigeria, Keshi alishinda tuzo ya kocha bora.