Sep 1, 2012

MASANJA MKANDAMIZAJI ATOA TAHADHARI

Mchekeshaji maarufu Tanzania ambaye pia ni muimbaji wa nyimbo za Injili Masanja au kwa jina jingine Mchungaji mtarajiwa, ametoa tahadhari kwa wanaom'beza kuigiza wakati yeye Mungu hajamwambia kuacha.

Msanii huyo ameyasema hayo hivi karibuni alipokuwa akihojiwa na mtangazaji maarufu Millard Ayo wa Clouds FM jijini Dar es salaam.

Hata hivyo hapo kabla Masanja aliwahi kunukuliwa kwamba ipo siku atakuwa mchungaji pia ataacha uigizaji Mungu atakaposema naye.

Mbali na hayo amewatangazia wanaouza CD feki kwamba “nimemaliza kufanya album yangu ya Gospel najua wako watu mamasta wa kuburn kazi za waimbaji nimewakaribisha waburn hii yangu, yani hamna kesi hashikwi mtu atakaeburn kazi yangu kwa sababu hii ni huduma ukiburn wauzie watu hata mia mia usiziweke ndani”

Kwenye sentensi nyingine Mchekeshaji huyu wa Orijino Komedi ya TBC1 amesema “kuna watu wananiambia Masanja tumeona watu wanauza CD feki nasema kama na wewe unaweza nunua na  ukatengeneze zako kwa sababu hii ni huduma nataka watu wapate ujumbe huu wabadilike wamjue Yesu tunaemuhubiri mwanawane”