Nov 8, 2012

PROFESSOR JAY FOUNDATION NA NISHIKE MKONO TOUR SOON KUANZA DAR

Msanii wa Bongo Fleva almaarufu kama Professor jay kwa hapa Tze anayetamba na ngoma zake kadhaa kali kama Hello,Nikusaidiaje,Kamiligado na nyinginezo kali sasa

Latest info ambayo tunayoifahamu kutoka kwa msanii huyu ni kwamba wiki iliyopita alikuwa akitoa misahada mbalimbali katika hospital ya Tumbi pamoja na mafunzo ya Elimu sasa leo amefunguka na kusema kwamba Professor Jay Foundation na Nishike mkono Tour inaendelea kwa hiyo watu wasidhani kwamba wamefanya tu maeneo ya Pwani kwani alifunguka na kusema kwamba ndiyo wapo katika mazungumzo na kamati nzima juu ya kutoa huduma za Afya na Elimu kwa hapa Dar es Salaam na akasema kwamba sehemu ambayo wamepanga kutoa huduma hizo ni maeneo ya Kigamboni siku ya tarehe 17 mwezi huu.Baada ya kusema hayo aliweza kuwa shukuru wale wote waliofika Pwani na kutoa kila ambacho wanacho.@Info by Professor jay...