Nov 6, 2012

Alichoandika Walter ktk Mitandao yake

"Nashukuru sana mtu wangu, ni Maombi na Kura zenu tuu.. Nashukuru kuingia FAINALI na nakuomba endelea na moyo huohuo kwa kunipigia kura kwa kuandika neno EBSS12 kwenda namba 15530".

Hiyo ni status aliyoiandika Walter katika ukurasa wake wa Facebook na Twitter jana baada ya kurushwa kwa show yake ya nusu fainali iliyompelekea kuingia fainali itakayofanyika Diomond Jubilee, Ijumaa ya tarehe 09/11/2012.

Pamoja na hayo Walter aliongeza kuwa anamshukuru Mungu na watanzania kwa hatua aliyofikia kwani haikuwa rahisi kihivyo.

Pia Walter ameongelea suala la yeye kuwa amnatokea Mbeya kwani ni jambo lililokuwa linachanganya watu wengi.

"Mimi ni mzaliwa wa Mbeya na naishi huko na mama yangu na wakati wa audition za EBSS nilikuwa nipo Dar katika michakato yangu na ndio sababu nikasailiwa kama mshiriki kutoka Dar".

Aliongeza, "Naomba watu wangu waendelee na moyo huo huo wa kuwa bega kwa bega na mimi na waendelee kunipigia kura kwani kura ndio kila kitu hata kama nitapendwa vip"

Walter ni mshiriki aliyeingia FAINALI pamoja na wenzake wanne, hivyo washiriki wa EBSS walio katika fainali ni Walter, Nshoma, Nsami, Wababa pamoja na Guiter gira Salma... 

Ili kumpigia kura Walter Chilambo, andika neno EBSS12 kwenda namba 15530".